2012-11-28 15:38:13

Wito wa Papa katika kuiadhimisha Siku ya Dunia dhidi ya Ukimwi.


Baba Mtakatifu, Jumatano hii amehimiza mashirika , taasisi na makampuni na watu wote duniani , kufanya kila jitihada za kutokomeza virus vya ukimwi duniani. Papa alitoa himizo Jumatano mchana wakati akihutubia mahujaji na wageni waliofika kusikiliza Katekesi yake ya Jumatano hii.

Papa aliukumbusha umati huo kwamba, tarehe Mosi Desemba ni Siku ya Dunia, inayoangalisha katika mapambano na maradhi ya Ukimwi, Maradhi yaliyoangamiza maisha ya watu wengi, licha ya kuwa adha kubwa na mateso kwa watu duniani , hasa kwa maskini na wanyoge zaidi duniani zaidi.

Na kwa namna ya pekee , Papa alielekeza mawazo yake kwa watoto ambao kila mwaka, mpka sasa wanapata maambukizi ya virusi kutoka kwa mama zao, licha ya uwepo uwezakano wa kuepusha na ambukizo hilo.

Katika kujali hilo, Papa ametoa ombi kwa mashirika na makampuni yote yanayoshughulika na changamoto hii ya kupambana na virusi, na katika mazingira ya utume wa kanisa Katika kazi ya zake kwa nyakati hizi, kufanikisha maisha ya furaha kamili kw afamilia kama jukumu upendeleo kwa familia , ambamo ndani yake, maisha ya imani inawezekana kuliishi kila siku kwa furaha, mazungumzo, kusameheana na kupendana. Papa amehimiza mipango mingi hata katika utume wa Kanisa, kwa ajili ya kukuzwa juhudi zaidi , katika kutokomeza janga hili.








All the contents on this site are copyrighted ©.