2012-11-28 10:15:03

Watanzania mlioko Diaspora jitokezeni kuchangia maoni kuhusu mustakabali wa Tanzania kupitia Katiba


Dr. James A. Msekela, Balozi wa Tanzania nchini Italia anaendelea kuwahimiza watanzania wanaoishi ughaibuni "diaspora" kujitokeza kwa wingi kuchangia maoni kuhusu mustakabali wa Tanzania kupitia Katiba, zoezi linalotarajiwa kukamilika ifikapo mwaka 2014. RealAudioMP3

Dr. Msekela anabainisha kwamba, Katiba ni Sheria Mama itakayokuwa na dhamana ya kuwaongoza Watanzania kwa miaka ijayo, kumbe, hili ni zoezi nyeti linawawajibisha kujitokeza ili kutoa maoni yao katika maeneo mbali mbali, lakini zaidi kuhusu uraia wa nchi mbili, kwani wao ndio watu wanaoguswa zaidi na dhana hii.

Maeneo mengine tete ni kuhusu: Imani, uhuru wa kuabudu na uhuru wa dhamiri; mambo yanayopaswa kuainishwa kikatiba.







All the contents on this site are copyrighted ©.