2012-11-28 15:21:04

Upendo wa Kristu umedhihirisha ukuu wa binadamu.


Katekesi ya Baba Mtakatifu Benedikto XV1, kwa Jumatano hii, imeendelea na Mada ya mwaka wa imani, na amezungumzia, namna tunavyoweza kumwasilisha Mungu katika nyakati hizi zetu. Kuiwasilisha imani ya Kikristu kama jibu la uhakika katika matamanio yote ya roho ya binadamu.
Papa anasema, hii inamaanisha kumpeleka Mungu wa Kristu kwa watu wote, wake kwa waume wa nyakati hizi zetu. Ni kushuhudia ujumbe wa Injili kupitia maisha manyenyekevu kila siku.
"Hii ni habari njema ya Mungu ambayo ni Upendo , unao tuwezesha sisi kuwa karibu na Yesu Kristu hata wakati wa vipindi vigumu vya majaribu ya Msalaba, na kwa Ufufuko wake, tunajazwa na tumaini na ahadi yake ya maisha ya milele. Yesu ni ishara ya upendo wake, unao jali haja za maisha na mahitaji yetu,mwenye kutuongoza kwa Baba ".
Papa aliendelea kusema , katika utume huu wa kumpeleka Mungu kwa watu wa nyakati hizi zetu, familia inakuwa ni nafasi nzuri, kupitia mfumo wake wa kifamilia, kuiishi imani katika maisha yake ya kila siku, yaliyo jazwa na tumaini na matazamio ya maisha ya milele, kwa furaha ya mazungumzano , msamaha na upendo.
Upendo wa Kristu ulio dhihirisha ukuu wetu kama watu waliokombolewa kwa upendo wake na kuitwa katika Kanisa, kuujenga mji mpya wa binadamu ili kwamba uweze kuwa ni Mji wa Mungu.









All the contents on this site are copyrighted ©.