2012-11-28 15:51:00

Mkutano wa Kimataifa 1V juu ya Uwasilishaji Urithi wa
Utamaduni.


Mkutano wa Kimataifa 1V juu ya mawasiliano katiak urithi wa utamaduni
Kwa muda wa siku tatu 5-7 Desemba 2012, katika jengo la Makumbusho la Vatican kutafanyika Mkutano wa Kimataifa wa 1V, ukiongozwa na Mada: "Jinsi gani inawezekana kuwasilisha urithi wa utamaduni katika jamii".
Kongamano hili la siku tatu, litaziduliwa na Antonio Paolucci, Mkurugenzi wa Majengo ya makubusho Vatican, pia atakuwepo Tullia Carettoni Romagnoli , Mjumbe na Rais wa shirika la Italia la Makumbusho la Herity , pia atakuwepo Kardinali Francesco Marchisano , Rais wa Tume ya Kimtaifa ya Herity.
....................................................................................................................
Na Jumanne 27 Novemba 2012, Kardinali Antonio Maria Veglia, alikutana na Wakurugenzi wa Kitaifa kwa ajili a kazi za kichungaji kwa wahamiaji na watu wasiolkuwa na makazimaalum kw aajili ya ufunguzi wa kazi za mkutano , kama ilivyoadaliwa na Baraza la Mabaraza ya Maaskofu ya Ulaya, utakao kamili tarehe 29 Novemba 2012. .
Kardinali Veglio, majira ya joni alizungumzia mada: "Mshikamano katika kazi za kichungaji kwa ajili ya Uinjilshaji mpya". Na majira ya jioni , katika ujengo la Domus Maria , Mtaa wa Aurelia 481, katika mazingira ya Mkutano huo, kulifanyika Ibada ya Misa .
Kardinali Antonio Maria Veglio , kwenye homilia yake , alionyesha kutambua haja ya kuwa na mbinu ya kweli na ubinadamu, kuanzia ndani ya kanisa lenyewe , katika utaratibu wake wa kuwapokea na kuwajali wahamiaji wanao “gonga" malangoni.

Alisema, hii inaonyesha kwa namna ya pekee jinsi Upendo wa Kristu unavyotakiwa kutimizwa , kwa maneno mengine ni “wito wa Kanisa kwa namna ya pekee kuwakarimu wahamaji na wenye shida , pia katika mitazamo na mipango ya kichungaji na majadiliano , lakini pia kusaidia waaminifu kuushinda moyo wa kujenga chuki na ubinafisi dhidi ya wageni wahamiaji.

Na hivyo ,ameutaja mkutano huu kuwa ni somo linaonyesha mwelekeo katika tafakari halisi za watu wanaohusika katika huduma ya kichungaji ya wahamiaji, kujenga ushrikiano na umoja katika katika kuhudumia.

Na alimalizia kwa kuomba msaada wa Roho Mtakatifu ili kwamba , ripoti ya wataalam, baada ya zoezi la kubadilishana mawazo na uzoefu, iweze kutoa mapendekezo mapya, katika huduma ya kichungaji ya wahamiaji. Na pia roho ya kukubali ushirikiano miongoni mwao, iweze kuelekeze katika mipango ya maendeleo ya thabiti na mbinu mpya ya uinjilishaji.







All the contents on this site are copyrighted ©.