Maaskofu wa Makanisa Katoliki ya Mashariki wakamilika mkutano wao.
Mkutano wa Maaskofu
wa Makanisa Katoliki ya Mashariki Ulaya, ulikamilika Jumatatu na azimio la Jinsi ya
kuboresha mchango wa Makanisa Katoliki ya Mashariki barani Ulaya. Hasa ufanikishaji
wa majadiliano ya kiekumeni sambamba na ongezeko la idadi ya wahamiaji kutoka Mashariki
ya Ulaya na Afrika wakiwemo waamini wa Makanisa Katoliki ya Mashariki. Na kwamba
Kanisa linapaswa kutambua mapungufu yake lenyewe, kuhusu mapokeo ya kiliturujia, kiteolojia
na Kiutamaduni.