2012-11-27 15:23:30

Kiko Urguello, mwanzilishi wa Ukatukumeni Mpya-atoa kitabu, jinsi alivyokutana na Kristu .


Kardinali Antonio Cañizares, Mkuu wa shirika kwa ajili ya Ibada Takatifu , katika utangulizi wa kitabu cha Kiko Uguello , Mwanzilishi wa njia ya Ukatukumeni Mpya "Neo-Catechumenal Way , amesema, juhudi hizo ni zawadi ambayo Roho Mtakatifu amelipatia Kanisa lake , kama njia ya majiundo mapya ya Mkristu, au kwa lugha nyingi mafundo mapya , na kama chombo cha kuhamasisha na kukuza uinjilishaji mpya"

"Kardinali amemshukuru Mungu kwa neema na maajabu makubwa yanayo endelea ndani ya Kanisa, kupitia njia hii ya Neo, ambamo kwa neema na baraka za Kanisa : Mama Kanisa anashuhudia matunda ya mabadiliko, ya maisha ya kikristo, na katika miito ya ukuhani na maisha yaliyowekwa wakfu, na kazi za kimisionari za Kanisa, kama matunda ya upendo, na maisha katika kutunza heri nane, ukarimu, na ya familia yenye maaisha ya kujifunua wazi, mmoja kwa mwingine.

Na Kardinali Christoph Schönborn, askofu mkuu wa Vienna, ikichangia maoni juu ya kuchapishwa kwa Kitabu cha Maisha ya Kiko Uguello, amekiita kitabu hicho kuwa ni mwaliko katika uongofu binafsi. Na kwamba, Katekesi zilizo chapishwa katika kitabu hiki zinavutia kwa sababu ya uwazi wake. Na hasa msisitizo kwamba , mimi binafsi, bila ya uongofu binafsi, haiwezekani kuinjilisha. Na hivyo kwa anayetaka kuinjilisha ni sharti ajiinjilishe yeye mwenyewe kwanza.
Mlei mwanzilishi wa Jumuiya ya Ukatukuemni mpya, "Neo Catechumenal Way", ametoa kitabu chake chenye maelezo binafsi jinsi alivyokutana na Yesu Kristu.








All the contents on this site are copyrighted ©.