2012-11-26 11:05:55

Wakatoliki Wakoptic wa Misri, kutazama mbinu za pamoja kukabiliana na upinzani.


Jumanne ya wiki hii, Ujumbe wa Kanisa Katoliki la Kikoptic nchini Misri , unatazamia kukutana na Patriaki Tawadros, Papa mpya wa Kanisa la kikoputic la Kiotodos aliyesimikwa rasmi, Jumapili ya tarehe 18 Novemba 2012.
Kwa mujibu wa Askofu Kyrillos William wa Assiust , ambaye pia ni Vika katika Upatriaki Katoliki wa Kikoptic, wa Misri, lengo la ziara ni kupata muda wa kushauriana jinsi wanavyoweza kuratibu kwa vizuri zaidi shughuli, za kanisa kwa nyakati hizi ambamo taifa la Misri linakabiliwa na machafuko ya kisiasa. Vurugu za upinzani na ghasia zilizoibuka , ambamo wapinzani wanataka uwezo wa Rais upunguzwe.
Kama ilivyokuwa wakati wa upinzani dhidi ya Rais Hosni Mbaraka , pia wakati huu wapinzani wamejazana katika uwanja wa Taharir, Cairo kudai demokrasia zaidi . Na Mashabiki wa Rais Morsi wanadai kwamba, kwa wakati huu ni muhimu Rais kuwa na uwezo zaidi, kwa ajili ya udumishaji wa mabadiliko ya kidemokrasia. Madai yanayotajwa na wapinzani kwamba , ni mwelekeo unaoongoza katika mfumo wa kidikteta, na kwamba Rais Morsi anataka kuwa Pharao Mpya.
Wiki iliyopita, wawakilishi wa jumuiya za Kikristu walijiondoa katika Baraza la Kikatiba, kama jibu kwa shinikizo linalotaka mabadiliko kwa mujibu wa makubaliano ya kikatiba.
Na Daima senti ya mjane maskini ni nguvu ya tumaini jipya – Burkina Faso.
Askofu Prosper Kontiebo , wa Jimbo Jipya Katoliki la Tenkodogo , Kusini mwa Mji wa Ouagadougou, Burkina Faso, ambaye amekuwa ni Askofu wa 400 katika historia ya shirika la Camellius, waliofika kwa mara ya kwanza , Oaugadougou, mwaka 1966, hivi karibuni, ameshuhudia jinsi senti ya mjane ilivyo na nguvu ya kumpa mtu tumaini jipya. Ushuhuda huo umeelezwa hivi karibuni na Padre Felice Rufini wa shirika la Wakamillioni, kwa shirika la Fides .
Askofu Kontiebo, aliishuhudia nguvu ya senti ya mjane, akirejea Injili ya Kristu, iliyosomwa Jumapili ya 32 ya mwaka , ambamo Yesu aliwatazama waliokuwa wakitoa sadaka , matajiri wakitoa kiasi kikubwa na mwanamke mjane kutoa senti mbili alizokuwa nazo (MK 12:41-44). Askofu anasema , senti hizo mbili, ni tumaini jipya alilopata pia, wakati alipo mtembelea bibi yake mkongwe, kwa nia ya kuaga kwamba, atakwenda Roma kukutana na Papa.
Bibi huyo mkongwe baada ya kusikia mjukuu wake anakwenda Roma kuonana na Papa, aliona ni nafasi pia kwake ya kutoa mchango wake kwa kazi za Papa, mara alinyanyuka na kuvuta kisanduku chake na kumpa kiasi cha franc 250 ambazo ni sawa na senti 38 za Euro, akisema, fedha hiyo ni mchango wake kwa Papa. Asema," kiasi hiki kidogo ninachokupa si chako, ila utakapofika katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro, ziweke katika kisanduku kilicho chini ya miguu yake Petro , kwa ajili ya Papa ".
Askofu anasema, mchango mdogo wa bibi huyu, unapaswa kumgusakila muumini wa kanisa katika nyakati hizi zetu, ambamo Kanisa linapambana na changamoto nyingi , lakini daima linamulikiwa na neema ya mwanga mkuu wa tumaini.








All the contents on this site are copyrighted ©.