Mwongozo kuhusu Kanuni ya Misa kwa Lugha ya Kiswahili
Hivi karibuni yalichapwa na kusambazwa majarida kwa ajili ya Kanuni Mpya ya Misa.
Majarida makubwa yalichapwa kwa ajili ya Mapadri Waadhimishi na majarida madogo yalitayarishwa
kwa ajili ya Mapadri Waadhimishaji Wenza na kwa ajili ya waamini kwa ajili ya kushiriki
maadhimisho ya ibada ya Misa. Tunaomba radhi kwa usumbufu, kumeonekana makosa
ya uchapaji na tafsiri katika majarida makubwa. Kwa hivi kumefanyika marekebisho
katika majarida makubwa na Idara ya Liturujia TEC imeamua kuchapa upya majarida hayo
kwa ajili ya Mapadri Waadhimishi. Uchapaji unatarajiwa kukamilika hivi karibuni.
Majimbo ambayo yalishanunua majarida makubwa, yatapelekewa majarida mapya bila malipo
mengine. Majimbo mengine yaendelee kuagiza majarida mapya kwa bei ile ile ya fedha
za kitanzania shilingi 3,000 tu kwa kila jarida kupitia anwani hii:
TMP BOOK
DEPARTMENT TABORA P.O.BOX 550 TABORA TANZANIA Tel. 0265097 / 026 2604244 e-mail:
tmpbookdept@yahoo.com
Majarida madogo yaliyotayarishwa kwa ajili ya Mapadri
Waadhimishi Wenza na Waamini yanaweza kutumika. Hata hivyo, tumeamua kuchapa upya
majarida hayo ili yaweze kuwa na maandishi yanayosomeka kirahisi zaidi na tena kupunguza
ukubwa wake ili iwe rahisi kushikika. Bei yake itatangazwa baadaye.
Tunawakumbusha
waamini wote kuwa kadiri ya Kanuni Mpya ya Misa viitikizano vya Misa vimebadilika.
Mfano:
Kiongozi wa ibada anaposalimia: Bwana awe nanyi, Wote wanaitikia:
Na awe rohoni mwako.
Katika gazeti la Kiongozi la ijumaa tarehe 16/11/2012
na ijumaa tarehe 23/11/2012 maelezo yametolewa kuhusu sababu za mabadiliko haya. Kwa
kifupi tafsiri mpya ya Misale ya Altare inazingatia Misale ya Altare ya kilatini: Mf.
Dominus vobiscum: Et cum spiritu tuo, maana yake Bwana awe nanyi: Na awe rohoni mwako.
Kanuni
Mpya ya Misa itaanza kutumika rasmi katika kanisa letu hapa Tanzania kuanzia tarehe
02. 12.2012 Jumapili ya kwanza ya Majilio.
Tunapenda kukumbusha pia muagize
KALENDA YA LITURUJIA zinazotengenezwa na Baraza la Maaskofu ambazo pia zi tayari.
Ni muhimu sana kuagiza kalenda zetu ili: kujua kwa undani maana na namna ya kuadhimisha
mafumbo mbali mbali katika mwaka wa kanisa, kujua matukio muhimu katika majimbo yetu,
kwa mfano, tarehe za kutabarukiwa makanisa ya jimbo, za kupata daraja ya uaskofu,
kumbukumbu ambazo zimeombewa hadhi ya kuwa sikukuu katika nchi yetu, n.k.
TUNAWATAKIA
USHIRIKI HAI KATIKA MAADHIMISHO YA IBADA YA MISA
Padri Paterni Patrick Mangi Katibu
Mtendaji Idara ya Liturujia, TEC.