Makardinali Wapya wapangiwa Makanisa ya huduma mjini Roma
Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, Jumamosi tarehe 24 Novemba 2012, baada ya
kuwasimika rasmi Makardinali wapya, aliwagawia pia Makanisa ambamo watayatumia kwa
ajili ya kutoa huduma ya kichungaji hapa mjini Roma. Kardinali James Michael Harvey:
atatoa huduma kwenye Kanisa la San Pio V kule Villa Carpegna. Kardinali Bechara
Boutros Rai O.M.M. Kardinal Baselios Cleemis Thottunkal, atakuwa mhudumu wa Kanisa
la San Gregorio VII. Kardinal John Olorunfemi Onaiyekan, atakuwa mhudumu wa Kanisa
la San Saturnino. Kardinal Ruben Salazar Gomez, atakuwa mhudumu wa Kanisa laSan
Gerardo Maiella. Kardinal Luis Antonio G. Tagle, atakuwa mhudumu wa Kanisa la San
Felice da Cantalice a Centocelle.