Ibada ya kusimikwa kwa Makardinali wapya sita, iliyoongozwa na Baba Mtakatifu Benedikto
wa kumi na sita, Jumamosi tarehe 23 Novemba 2012, imehudhuriwa na wawakilishi maalum
kutoka Lebanon, ujumbe ambao umeongozwa na Jenerali Michel Sleiman, Rais wa Lebanon.
Kutoka nchini Ufilippini, ujumbe umeongozwa na Bwana Jejomar C. Binay, Makamu wa Rais
wa Ufilippini.
Ujumbe wa waamini na watu wenye mapenzi mema kutoka India,
umeongozwa na Profesa P. J. Kurien, Rais wa Bunge la India. Kwa upande wa Kardinali
John Onayeikan, ujumbe kutoka Nigeria uliongozwa na Seneta David Mark.
Licha
ya kuhudhuria Ibada ya kusimikwa kwa Makardinali wapya, wawakilishi hawa pia watashiriki
katika Ibada ya Misa Takatifu, Maadhimisho ya Sherehe ya Kristo Mfalme, ambayo Baba
Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita pamoja na Makardinali hawa wapya wataongoza Ibada
ya Misa Takatifu.