2012-11-24 11:14:04

Vijana wa Taizè kukutana Roma kuanzia tarehe 28 Desemba hadi tarehe 2 Januari 2013


Jumuiya ya Kiekumene ya Vijana wa Taizè kwa kushirikiana na Jimbo kuu la Roma pamoja na Idara ya shughuli za kichungaji kwa vijana, kuanzia tarehe 28 Desemba hadi 2 Januari 2013, watafanya mkutano wao wa thelathini na tano mjini Roma, kwa kuwashirikisha vijana kutoka sehemu mbali mbali za Bara la Ulaya, ambao watashiriki hija ya imani duniani.

Hii ni sehemu ya utekelezaji wa Maadhimisho ya Mwaka wa Imani uliozinduliwa hivi karibuni na Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita. Mkutano huu kwa namna ya pekee, itakuwa ni fursa kwa vijana kujichotea utajiri wa upendo unaobubujika kutoka katika tafakari ya kina na sala zitakazoendeshwa kwenye Makanisa Makuu yaliyoko mjini Roma.

Ratiba inaonesha kwamba, tarehe 29 Desemba 2012, Jioni, Vijana wa Taizè watakutana na kusali pamoja na Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, kwenye Kanisa kuu la Mtakatifu Petro, mjini Vatican. Vijana hawa ni kielelezo cha mshikamano wa dhati unaofumbata tunu msingi za maisha ya kiroho, kama ilivyojionesha hivi karibuni nchini Rwanda ambako vijana elfu nane na mia tano, kutoka katika nchi thelathini na tano. Inawezekana kabisa watu wakaishi kwa umoja, upendo na mshikamano, licha ya tofauti zao za kiimani.







All the contents on this site are copyrighted ©.