2012-11-22 08:41:44

Maaskofu Marekani wachangia fedha kwa ajili ya mikakati ya shughuli za kichungaji Amerika ya Kusini; kielelezo cha mshikamano wa upendo na kidugu


Baraza la Maaskofu Katoliki Marekani katika mkutano wao uliohitimishwa hivi karibuni wamepitisha jumla ya miradi mia moja na sitini, yenye thamani ya dolla za kimarekani zipatazo millioni 2.3, itakayotolewa kwa ajili kugharimia miradi ya shughuli za kichungaji inayofanywa na Kanisa Amerika ya Kusini.

Hiki ni kielelezo cha mshikamano wa upendo, kwa Kanisa Amerika ya Kusini ambalo kwa siku za hivi karibuni limetikiswa na majanga asilia yaliyosababisha maafa na uharibifu mkubwa wa mali na miundombinu.

Fedha hii ya msaada itatumika kugharimia miradi iliyokoHaiti, Chile na Cuba. Lengo ni kusaidia ujenzi wa miundombinu ya Makanisa yaliyoharibiwa hivi karibuni na tufani ya Sandy pamoja na miradi mingine inayopania kuimarisha shughuli za: majiundo ya viongozi wa Kanisa pamoja na nchi ambazo zitashiriki katika maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani kwa mwaka 2013, itakayofanyika nchini Brazil.







All the contents on this site are copyrighted ©.