Monsinyo Josè Avelino Bettencourt ateuliwa kuwa Kiongozi Mwandamizi wa Itifaki mjini
Vatican
Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, amemteua Monsinyo Josè Avelino Bettencourt,
kuwa Kiongozi Mwandamizi wa Itifaki mjini Vatican. Kabla ya uteuzi wake alikuwa ni
mshauri wa Balozi za Vatican. Alizaliwa tarehe 23 Machi 1962 mjini Azzorre, Ureno.
Baada ya masomo na majiundo yake ya kikasisi, alipadrishwa tarehe 23 Juni
1993 kwa ajili ya Jimbo kuu la Ottawa, Canada. Alianza kutoa huduma za kichungaji
mjini Vatican hapo tarehe Mosi, Julai 1999. Amewahi kutekeleza majukumu na utume wake
kwenye Balozi za Vatican nchini DRC na baadaye alijereshwa tena mjini Vatican kuendelea
na utume wake katika kitengo cha mambo ya nchi za nje na uhusiano wa kimataifa.