Maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani, Rio de Janeiro, 2013
Kamati ya Maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Vijana Duniani itakayofanyika kuanzia
tarehe 23 hadi 27 Julai 2013, huko Rio de Janeiro, imebainisha kwamba, Serikali ya
Brazil, imesema kwamba, kwa mahujaji wote watakaoshiriki katika maadhimisho ya Siku
ya Vijana Kimataifa hawatalazimika kupata hati ya kuingilia nchini humo.
Ili
kufanikisha dhamana hii, mahujaji watalazimika kujaza fomu maalum inayotolewa na Wizara
ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa; watatakiwa kuwa na hati za kusafiria pamoja
na hati ya utambulisho kutoka Kamati ya Maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Vijana
Duniani kwa mwaka 2013.
Mahujaji watakaoshiriki katika Maadhimisho ya Siku
ya Vijana Duniani wanaruhusiwa kuendelea kwenda mjini Rio de Janeiro hadi tarehe 28
Julai 2013. Hati ya kusafiria itadumu kwa siku tisini. Na wale ambao watakuwa wamechaguliwa
kwa kazi ya kujitolea wanaweza kuishi nchini Brazil kwa kipindi cha mwaka mmoja.