Papa ateuwa viongozi wa Taasisi Mpya ya Lugha ya Kilatini
Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, amemteua Profesa Ivano Dionigi kuwa Rais
wa Taasisi ya Lugha ya Kilatini. Wakati huo huo, Mheshimiwa Padre Roberto Spataro
ameteuliwa kuwa Katibu mkuu wa Taasisi hii inayopania kukuza na kuendeleza lugha ya
Kilatini ndani ya Kanisa.
Uteuzi wao utadumu katika kipindi cha miaka mitano.
Taasisi hii itakuwa ni jumla ya wakufunzi na wasomi wasiopungua hamsini, watakaoteuliwa
na Katibu mkuu wa Vatican.