2012-11-08 08:30:13

Vatican na Burundi kushirikiana kwa ajili ya mafao ya wananchi wa Burundi


Askofu mkuu Franco Coppola, Balozi wa Vatican nchini Burundi kwa niaba ya ujumbe wa Vatican ameweka sahihi kwenye Mkataba wa Ushirikiano kati ya Vatican na Burundi, kwa ajili ya mafao ya nchi hizi mbili. Waziri wa Mambo ya nchi za nje na ushirikiano wa kimataifa Laurent Kavakure alitia sahihi kwa niaba ya Serikali ya Burundi, tukio ambalo limehudhuriwa na Rais Pierre Nkurunziza wa Burundi.

Mkataba huu unapania kuendeleza na kudumisha uhusiano wa kidiplomasia uliofikiwa kati ya Vatican na Burundi kwa takribani miaka hamsini iliyopita. Mkataba pamoja na mambo mengine, unatoa uhakika wa kisheria kwa Kanisa katika masuala mbali mbali, yakiwemo: ndoa zinazofungwa ndani ya Kanisa Katoliki, maeneo ya Ibada na sala; Taasisi za elimu, afya na maendeleo endelevu; ufundishaji wa dini shuleni, huduma za kijamii, huduma za maisha ya kiroho kwenye vikosi vya ulinzi na usalama, magereza na hospitali. Mktaba huu utaanza kutumika pale utakaporidhiwa na pande hizi mbili.







All the contents on this site are copyrighted ©.