2012-11-06 07:52:59

Unganisheni nguvu kuokoa maisha ya watoto chini ya miaka 5 wanaofariki dunia kutokana na baa la njaa Kusini mwa Jangwa la Sahara


Baa la njaa Barani Afrika linaendelea kuwa ni chanzo kikuu cha vifo vya watoto wengi wenye umri chini ya miaka mitano, Kusini mwa Jangwa la Sahara. Hii ni kutokana na uwepo wa utapiamlo wa kutisha unaosababishwa kwa namna ya pekee na: ukame wa muda mrefu pamoja na mfumuko wa bei za mazao ya chakula. Ukosefu wa chakula na lishe bora kwa watoto wenye umri wa miaka mitano, umepelekea watoto hawa kudumaa na matokeo yake ni kushindwa pia katika masomo.

Taarifa hii imetolewa hivi karibuni wakati wa maadhimisho ya Siku ya Lishe na Usalama wa Chakula Barani Afrika. Katika maadhimisho haya, wadau mbali mbali waliziomba Serikali, wahisani na vyama vya kiraia kuunga mkono juhudi za kupambana na baa la njaa Barani Afrika, kama njia ya kuokoa maisha ya watoto wenye umri chini ya miaka mitano.







All the contents on this site are copyrighted ©.