2012-11-06 09:32:19

Kongamano la Shirikisho la Wasalesiani kufanyika mjini Roma kuanzia tarehe 8 hadi 11 Novemba 2012


Shirikisho la Wasalesiani Kimataifa, lililoanzishwa kunako mwaka 1876 na Mtakatifu Yohane Bosco, linalowajumuisha: waamini walei, watawa na makleri, litakuwa na Kongamano la Kimataifa, kuanzia tarehe 8 hadi 11 Novemba 2012 hapa mjini Roma.

Kongamano hili linawashirikisha wajumbe mia tatu kutoka katika ngazi mbali mbali: kitaifa na kimataifa. Mkutano huu unaongozwa na kauli mbiu: Mradi wa maisha ya kitume: kwa njia ya uaminifu kwa karama ya Mtakatifu Yohane Bosco. Lengo ni kutaka kupembua na hatimaye, kupitisha Katiba ambayo itakuwa ni dira na mwongozo katika maisha na utume wao ndani ya Kanisa, katika mapambazuko ya Millenia ya tatu ya Ukristo. Wajumbe watapata fursa ya kumchagua Mratibu mkuu, atakayeongoza Shirikisho hili kwa muda wa miaka sita.

Shirikisho hili limekuwa ni kielelezo cha ushuhuda makini unaotolewa na wanachama wake katika medani mbali mbali za maisha ya Kanisa na Jamii katika ujumla wake. Lakini wanachama ambao wanatambulikana kutokana na mchango wao makini katika sekta ya elimu, maendeleo jamii, siasa na utume wa Uinjilishaji miongoni mwa vijana wa kizazi kipya.







All the contents on this site are copyrighted ©.