2012-11-05 11:08:17

Vitendo vya kigaidi bado vinajitokeza nchini Kenya


Kwa siku za hivi karibuni Kenya imeendelea kuwa ni uwanja wa vitendo vya kigaidi vinavyohatarisha amani, utulivu na usalama wa nchi. Jumapili iliyopita, mtu mmoja alipoteza maisha na wengine kumi na moja wamejeruhiwa vibaya baada ya kulipukiwa na bomu lililotupwa karibu na Kanisa eneo la Garissa linalopakana na Somalia. Baadhi ya wachunguzi wa mambo wanabainisha kwamba, tukio hili linavionjo vya kisiasa zaidi kuliko kinzani za kidini.

Tangu Kenya ilipoamua kulivalia njuga tatizo la vitendo vya kigaidi vilivyokuwa vinafanywa na Kikundi cha Al Shebaab kutoka Somalia, imejikuta mara nyingi ikitikiswa kwa vitendo vya kigaidi. Itakumbukwa kwamba, Mwezi Julai, 2012, Makanisa mawili yalilipuliwa katika eneo la Garissa na kusababisha watu 18 kupoteza maisha yao. Matukio ya kigaidi hata kwa siku za hivi karibuni yamejionesha Nairobi.







All the contents on this site are copyrighted ©.