2012-10-30 08:20:06

Vatican na Croatia kuendelea kushirikiana kwa ajili ya mafao ya pande hizi mbili


Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, Jumatatu tarehe 29 Oktoba 2012 amekutana na kufanya mazungumzo na Bi Zoran Milanovic, Waziri mkuu wa Croatia pamoja na ujumbe wake. Viongozi hawa wawili wametumia fursa hii kubadilishana mawazo na changamoto ambazo Croatia inakabiliana nazo kwa wakati huu kutokana na athari za myumbo wa uchumi kimataifa. Wamegusia masuala yenye mafao kwa pande hizi mbili.

Wamezungumzia pia kuhusu Kongamano lililoandaliwa na Croatia kwa kushirikiana na Vatican kama sehemu ya kumbu kumbu ya maadhimisho ya Miaka ishirini ya uhusiano kati ya Vatican na Croatia, lililofanyika Jumatatu tarehe 29 Oktoba, 2012. Viongozi hawa pia wamekubaliana kimsingi kulipatia ufumbuzi tatizo la Dajla katika hali ya mapokeo ya kirafiki kati ya Vatican na Croatia.

Baba Mtakatifu amemhakikishia mgeni wake kwamba, Vatican itaendelea kuunga mkono jitihada zinazolenga kuiwezesha Croatia kujiunga na Umoja wa Ulaya, bila kusahau hali halisi ya wananchi wa Croatia walioko Bosnia na Erzegovina.

Waziri mkuu Zoran Milanovic na ujumbe wake, walipata pia fursa ya kukutana na viongozi waandamizi kutoka Vatican chini ya uongozi wa Kardinali Tarcisio Bertone, Katibu mkuu wa Vatican.







All the contents on this site are copyrighted ©.