2012-10-29 11:16:02

Vatican na Croatia zafanya kumbu kumbu ya miaka 20 ya uhusiano wa Kidiplomasia kwa Kongamano na Hija ya Kiroho mjini Roma


Baraza la Maaskofu Katoliki Croatia, katika mkutano wake uliohitimishwa hivi karibuni, pamoja na mambo mengine limejadili kuhusu kumbu kumbu ya maadhimisho ya miaka ishirini tangu Croatia na Vatican zilipoanzisha uhusiano wa kidiplomasia. Mkutano huu umehudhuriwa pia na Askofu mkuu Alessandro D'Errico, Balozi wa Vatican nchini Croatia.

Maaskofu wamezungumzia kuhusu hija ya kikazi itakayofanywa na Waziri mkuu wa Croatia Bwana Zoran Milanovic pamoja na kushiriki katika Kongamano litakalojadili kuhusu uhusiano wa kidiplomasia kati ya Vatican na Croatia katika kipindi cha miaka ishirini iliyopita; kongamano ambalo linafanyika hapa mjini Vatican tarehe 29 Oktoba, 2012.

Baraza la Maaskofu Katoliki Croatia litafanya hija ya kichungaji mjini Roma, ili kumshukuru Mungu kwa matunda ya uhusiano uliopatikana kati ya nchi hizi mbili pamoja na kuadhimisha Mwaka wa Imani, uliotangazwa na kuzinduliwa na Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, hivi karibuni.







All the contents on this site are copyrighted ©.