Jumatano hii, Baba Mtakatifu Baada ya Katekesi yake kwa mahujaji na wageni, pia alitangaza
majina ya sita ya Makadinali wapya wateule, watakaotajwa rasmi wakati wa Baraza la
Makadinali hapo Novemba 24, 2012. Makardinali wapya wateule ni Mons.JAMES
MICHAEL HARVEY, Padre Mkuu wa Kanisa la Kipapa la Mtakatifu Paulo nje ya kuta Roma. Mwenye
Heri BÉCHARA BOUTROS RAÏ, Patriarca wa Antiochia ya Maroniti (Lebanon); Mwenye
Heri BASELIOS CLEEMIS THOTTUNKAL, Askofu Mkuu wa Trivandrum ya Siro-Malankaresi
(India); Askofu Mkuu JOHN OLORUNFEMI ONAIYEKAN,wa Jimbo Kuu la Abuja (Nigeria); Askofu
Mkuu RUBÉN SALAZAR GÓMEZ, wa Jimbo K uu la Bogotà (Colombia); Na Askofu Mkuu
LUIS ANTONIO TAGLE, wa Jimbo kuu la Manila (Filippine). Papa alitangaza na kuwaomba
waamini watolee sala zao kwa ajili ya Makardinali wapya, kuomba msaada kwa Mama Bikira
Maria , ili waweze kulipenda kanisa kwa ushupavu na majitoleo kwa ajili ya Yesu Kristu
na Kanisa lake.