2012-10-23 15:51:06

Katekesi ni muhimu katika majiundo na ukomavu wa imani kwa wafuasi wa Kristu


Hili ni wiki la Mwisho la Sinodi ya Maaskofu kwa ajili ya Uinjilishaji mapya. Jumatatu kazi za Sinodi kwa ajili ya Uinjilishaji mpya , zilifanyika katika hali ya faragha, kwa ajili ya uunganishaji mawazo na mapendekezo yaliyo kwisha tolewa. Sinodi inafungwa jumapili ya wiki hii, 28 Oktoba kwa Ibada ya Misa.

Taarifa zinasema, michango mbalimbali ya maoni na ushauri iliyotolewa na Mama katika siku hizi za Sinodi, imeonyesha umuhimu wa juhudi mpya katika Uinjilishaji kuangalishwa kwa watu wazima pia , ambao wengi wameonekana au mwelekeo wa kusahau jukumu lao, kama waamini kuirithisha misingi ya imani, elimu na shuhuda, kwa kizazi kipya cha vijana.

Na kwa namna pekee , Mons. Satanislaw Gadecki wa Poland, alitoa uzoefu wa shule ya Katekesi ya watu wazima ,kama sehemu ya uinjilishaji mpya, nchini mwake. Na kwamba mpaka sasa bado wanashakia kuchukua hatua ya kutoa katekesi kwa watoto na vijana, kabla ya kuwakiria kwanza watu wazima, kwa dhana kwamba, katekesi kwa watoto, itakwua ni matunda na maendeleo ya Katekesi kwa watu wazima.

Na ameasa kwamba, mafanikio katika makundi yote mawili, watu wazima na vijana, yanategemea sana watu wazima wenyewe , tabia na maisha yao. Kwa mara nyingi, imani haba kwa mtu mzima huharibu pia mbengu nzuri ya Imani iliyo pandikizwa kwa vijana. Uenezaji wa Imani na utendaji wake , usitokana na iamni yamtu mzima , kwa vijana hutoweka mara.

Aidha Mons. Stanslaw Gadecki ameonyesha kujali jinsi watu wazima wanavyokosa muda wa kukakaa na watoto wao, kutokana na hali halisi za ukali wa maisha, kwamba, watu wazima wanalazimika kuishi maisha ya uchugu wa kufanya kazi kwa muda mrefu zaidi, ili kukidhi mahitaji ya familia. Wengi badala ya saa nane, wanafanya zaidi ya saa 12 au hata 14 kwa siku, na hivyo hurejea nyumbani jioni wamechoka na hawana muda wa kukaa na watoto wao, kuwaelimisha yale wanaoyajua ikiwemo imani yao.

Pamoja na changamoto hii, kwa ajili ya kuimarisha uelewa wa imani kwa watu wazima ili waweze kuirithisha kwa watoto wao, inakuwa ni jambo muhimu kutoa Katekesi kwa watu wazima. Na hiyo ndilo lengo la shule ya makatekista walei, na watu wazima , kupata uzoefuzaidi katika imani yao na kujenga ukomavu unaostahili.
Na kwamba wameanzisha shule ya Katekesi kwa watu wazima , baada ya kugundua kwamba haiwezekani kuwa na Makatekista na shuhuda thabiti bila ya maandalizi. Na uzoefu umeonyesha kwamba, lugha ya walei katika kuieneza imani kwa watu wazima walei ina shawishi zaidi, kuliko lugha ya Mapadre.








All the contents on this site are copyrighted ©.