2012-10-22 15:45:16

Chagua kiongozi bila ya kujali dini, kabila au mahusiano - Kasisi ahimiza.


Jambo la kwanza kabisa katika kumfikiria kiongozi bora ni uadilifu wake katika kuainisha dini na siasa. Na hamu za kumchagua kiongozi asiyekuwa mwaminifu eti kwa sababu tu ni wa dini yako, hiyo ni dhambi kwa dini ya kweli. Ni wito uliotolewa na Padre Wilybard Lagho, Kasisi wa Mombasa na Rais wa Baraza la Pwani linalo waunganisha wakuu wa dini (CCC), katika kutafakari juu ya uchaguzi ujao wa urais utakao fanyika nchini Kenya mwaka ujao.

Padre Lagho ameitaja nafasi ya uchaguzi, kuwa fursa kwa wapiga kura , kuchagua viongozi waaminifu, bila kujali hadhi yai kifedha, kabila au dini au mahusiano. Ameuita uchaguzi wa viongozi wa kisiasa, kuwa mtihani wa uadilifu kwa wapiga kura wenyewe.
Maelezo ya Padre Lagho yamenukuliwa na shirika la Fides, ambamo amerejea kumbukumbu ya mapigano ya hivi karibuni, yaliyogusa madhehebu ya kidini mjini Mombasa. Fr. Lagho, amesema , Koran na Biblia, vyote huwataka Wakristo na Waislamu kuishi kwa amani na ujirani mwema.

Na kwamba, ni jambo lisilo wezekana sasa , kwa ukanda wa pwani, hasa katika jiji la Mombasa, ambako Waislamu na Wakristo, wameishi karne hadi karne kwa hali ya utulivu na amani licha ya tofauti za kidini, sasa kuibua utengano, kati ya jumuiya hizi mbili. Ameeleza na kurejea maelezo ya Mtume Mohammed juu ya jirani mwema kwamba, Jibrael (Gabriel) alipendekeza kuwahudumai majirani kwa wema na upole(Sahih Bukhari zote - kitabu cha Ahkaam). "

Na kwa mfano wa Msamaria mwema uliotolewa katika Kitabu cha Injili, Wakristu wanafundishwa kuwahudumia majirani na maskini bila kujali itikadi zao za kijamii, kikabila na kidini (Luka 20, 25-37)."

Padre Lagho alimalizia ujumbe wake kwa kuwataka viongozi wa dini, kuungana na kuhamasisha wapiga kura kuchagua viongozi waaminifu ambao watafanikisha watu wengi zaidi kufurahia uhuru wao dhidi ya minyororo ya rushwa na mafisadi










All the contents on this site are copyrighted ©.