Balozi Carl-Henri Guitea awasilisha hati zake za Utambulisho mjini Vatican
Askofu mkuu Dominique Mamberti, Katibu mkuu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
mjini Vatican, tarehe 18 Oktoba 2012 amepokea hati za utambulisho kutoka kwa Mheshimiwa
Carl-Henri Guiteau, Balozi mpya wa Haiti mjini Vatican.
Itakumbukwa kwamba,
kunako tarehe 6 Julai 2012, Mheshimiwa Balozi Guiteau aliwasilisha hati zake za utambulisho
kwa Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, kama mwakilishi maalum wa Haiti mjini
Vatican.