Tanzania na Oman zina mahusiano ya kidamu na kindugu ambayo ni maalum sana yanayopaswa
kudumishwa, kuthaminiwa na kuenziwa kwa dhati. Rais Jakaya Mrisho Kikwete amemwambia
Mfalme Qaboos Bin Said katika mazungumzo rasmi yaliyofanyika katika nyumba ya kifalme
ya Al -Alam mara baada ya kuwasili katika Taifa la Kifalme la Oman hapo tarehe 15
Oktoba 2012, kuanza ziara ya kiserikali ya siku 4. "Tanzania na Oman zina mashirikiano
maalum kuliko nchi nyingine yeyote duniani kwa sababu ya undugu wa damu uliopo baina
ya watanzania na wa Oman, hivyo hii ni ziara maalum sana katika nchi zetu." Rais
amemwambia Mfalme. Mfalme Qaboos amekubaliana na Rais Kikwete na kumueleza kuwa ni
muhimu mahusiano haya yakadumishwa zaidi kwa njia ya uwekezaji katika nyanja mbalimbali,
hasa katika Viwanda. Rais Kikwete amepokelewa rasmi kwa kupigiwa mizinga 21 na
kuandaliwa chakula maalum cha usiku ambapo Rais na ujumbe wake wamehudhuria. Katika
ujumbe wake Rais amefuatana na Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Tanzania Mhe. Bernard
Membe, Waziri wa Nishati na Madini Mhe. Prof Sospeter Muhongo, Waziri wa Biashara
na Viwanda Mhe. Dr. Abdallah Kigoda, Waziri wa Kazi, Ushirika na Uwezeshaji , Zanzibar
Mhe. Haroun Ali Suleiman na Naibu Waziri Fedha wa Tanzania Mhe. Janet Mbene. Katika
Ziara hii, Rais amefuatana na wafanyibiashara kutoka Tanzania Bara na Zanzibar ambapo
tarehe 16 Oktoba,2012 anafanya kikao na wafanyabiashara wa Tanzania na Oman na hatimaye
kutia saini makubaliano ya kibiashara na kiuchumi baina ya nchi mbili hizi. Mbali
na kufanya mkutano na wafanyibiashara, leo Rais atatembelea makumbusho ya jeshi na
jioni atakutana tena na Mfalme kwa ajili ya chakula binafsi cha