2012-10-15 10:50:41

Wakristo simameni kidete kulinda mali zenu pamoja na kutetea haki zenu msingi dhidi ya nyanyaso na madhulumu ya kidini!


Askofu Mkuu Josephat L. Lebulu wa Jimbo Kuu Arusha, Tanzania amewataka watanzania kwa namna ya pekee kujitokeza kuchangia maoni yao katika mchakato wa Katiba Mpya ya Tanzania, kama sehemu ya utekelezaji wa dhamana yao kama raia wa Tanzania.

Askofu Mkuu Lebulu amesikitishwa sana na vitendo vya dhuluma na uvunjifu wa misingi ya uhuru wa kuabudu, haki na amani vinavyoendelea kujitokeza nchini Tanzania, licha ya Kanisa kuongeza jitihada za kukuza na kudumisha majadiliano ya kidini na kukazia umuhimu wa kufuata na kuzingatia utawala wa sheria, lakini haki, amani na utulivu sanjari na mustakabali wa taifa, vimeendelea kuwekwa rehani na baadhi ya Waamini wachache wanaoendeleza sera za ubabe na nguvu dhidi ya Wakristo nchini Tanzania.

Askofu Lebulu anawataka sasa Wakristo nao kusimama kidete kupinga dhuluma na nyanyaso na ukosefu wa misingi ya haki wanayotendewa nchini Tanzania kwa kuhakikisha kwamba, haki yao ya kuabudu inaheshimiwa na kuthaminiwa na Waamini wa dini nyingine nchini humo. Kanisa haliwezi kukaa kimya na kuona watu wanadhulumiwa na mali yake inateketea kwa visingizio vya udini. Zaidi anafafanua kama ifuatavyo: RealAudioMP3







All the contents on this site are copyrighted ©.