Kitengo cha Uchapishaji cha Vatican, kwa mara nyingine tena kinashiriki katika Maonesho
ya Vitabu, yaliyofunguliwa rasmi huko Frankfurt, Ujerumani kuanzia tarehe 10 hadi
tarehe 14 Oktoba, 2012. Kitengo hiki kinashirikisha zaidi ya vitabu elfu sita. Katika
banda la Vatican kuna machapisho pia kutoka Baraza la Maaskofu Katoliki Marekani.
Machapisho kuhusu Mwaka wa Imani uliozinduliwa rasmi na Baba Mtakatifu Benedikto
wa kumi na sita, tarehe 11 Oktoba 2012 yana umuhimu wa pekee katika maonesho haya.
Kuna vitabu vinavyozungumzia pia Uinjilishaji mpya, maisha ya kiroho na tafakari za
kina zinazotolewa na Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita.