2012-10-10 14:57:55

Uinjilishaji mpya si tu kauli mbiu....


Jumanne Asubuhi, mbele ya Papa na Maaskofu kutoka dunia nzima, Sinodi ilifunguliwa na wito wa amani Syria. Na pia kuliwasilishwa matatizo yadhuluma kwa wahamiaji na umuhimu wa kuchunguza dhamiri ya Kanisa, na njia za kuiishi imani.

Wajumbe wa sinodi, wakitazama changamoto dhidi ya uinjilishaji mpya, waliomba msaada wa kulindwa kwa wakimbizi na makundi madogomadogo dhidi ya aina fulani ya ubaguzi katika jamii na kuwezesha ushirikiano na utunzaji wa utambulisho wao wa Kikristu


Sinodi pia ilikosoa madhulumu yanayofanywa na makuhani na kuomba uchunguzi wa kidhamiri katika mna za kuishi na kuwa mashahidi wa imani duniani na katika kuonyesha maana halisi ya sakramenti katika uinjlishaji mpya, mkitajwa hatari za urasimu katika maisha ya kisakramenti kwamba huhatarisha imani kupotea. Ni muhimu basi,Uinjilishaji mpya wa Kanisa ufanyike kwa uneynyekevu mkuu na si katika mitazamo ya kujifungia katika mijadala ya ndani ya makanisa , lakini kuitagaza Injili kwa unyenyekevu , katika mwanga wa huduma mpya.

Pia ni muhimu kwa watumishi wa kanisa waliochukua dhamana ya ukuhani, kujiepusha au kurudia kashfa za madhulumu hasa kwa wau wanyonge kama watoto, na kupambana na vipingamizi vingine, kama haja ya kidharura, kupitia njia ya uelimishaji.Sinodi imeonya ni wazi hakuna uinjlishaji kama muinjilishaji mwenyewe anaishi kinyume cha Injili anayoitangaza.

Na Jumanne mchana, Maaskofu walisikiliza ripoti zilizowasilishwa kutoka mabara matano, zikionyesha jinsi mandhari ya uinjilishaji mpya , imepokelewa duniani kote. Kwa ujumla ripoti hizo zilionyesha kuwa na tatizo linalofanana changamoto ya utandawazi, ambao imekuwa na mwelekeo wa kubadilisha tamaduni mahalia na kudharirisha maadili ya kijadi, kama familia.


Na kwa namna ya pekee zilitazamwa kazi za uinjilishaji barani Asia, kama hitaji msingi na si doto ya kufikirika katika kuzitazama hali halisi za maisha ya Wakristu na jamii kwa ujumla kitamaduni, kihali na kidini, ikiwa ni pamoja na kushughulikia mateso ya kishujaa ya wanaoiishi imani yao ya Kikristu.

Afrika, kwa upande wake, mapambano dhidi ya ubabe wa waislamu wasiovumilia wengine, yalitazmwa kwa makini, ikiwemo mafundisho ya Papa Paulo VI, yaliyowataka " Waafrika, kusimamam imara na kujiijilisha wenyewe kwa wenyewe". .









All the contents on this site are copyrighted ©.