2012-10-10 14:38:34

Papa asikitishwa na binadamu wanaomsahau Mungu .


Baba Mtakatifu Benedikto XV1, akiwahutubia mahujaji na wageni , waliofika kumsikiliza Jumatano hii mjini Vatican, aliyarejea matukio mawili yanayozinduliwa wiki hii , yanayokwenda sambamba, kufunguliwa kwa maadhimisho ya miaka 50 ya Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican na kuanza kwa mwaka wa Imani.
Papa akiwa mmoja wa Mababa walioshiriki Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican, amezikumbuka vyema, shauku, tumaini na furaha, si tu ya Maaskofu, lakini ya Kanisa zima Katika kipindi hicho.
Ameonyesha tumaini lake kwamba, tunapoanza Mwaka wa Imani, unao zinduliwa Alhamis hii 11 Oktoba 2012, inakuwa ni muhimu kurejea nyaraka za mkutano huu muhimu, kama alivyoeleza Mwenye Heri Yohana XXIII, kutangaza ukweli wa imani, kwa njia mpya , bila kubadili maudhui yake.
Aliendelea kufundisha kwamba, nyakati hizi zetu zilizomsahau Mungu, kunahitaji kukumbusha tena ujumbe mkuu wa Baraza, kwamba, Ukristo ni imani kwa nafsi tatu za Mungu mmoja, Baba Mwana na Roho Mtakatifu. Na ni kukutana kama mtu binafsi au jumuiya na Kristu , mwenye kubadili na kutoa maana ya maisha . Mengi yote hutoka kwake.
Papa aliomba, kama ilivyokuwa wakati wa Baraza, pia katika wakati wetu huu, tuweze kutambua kwa uwazi kwamba, Mungu yupo , na anatuangalia , na kutujibu , na wakati binadamu anapomsahau Mungu, husahau jambo muhimu katika ubinadamu wake mwenyewe.
Hivyo basi Maadhimisho ya miaka hamsini wa Mtaguzo Mkuu wa Pili, na yanakumbusho hilo kwamba, Kanisa, na waamini wake wote, wana wajibu wa kueneza ujumbe wa upendo wa Mungu wa kuokoa, unaoongoza katika Heri ya milele.








All the contents on this site are copyrighted ©.