2012-10-08 14:47:36

Sinodi ya kawaida ya 13 ya Maaskofu kwa ajili ya Uinjilishaji Mpya yaanza Vatican


Mapema Jumatatu wajumbe wa Mkutano wa Sinodi ya Kawaida ya 13 ya Maaskofu, waliianza ratiba ya sinodi hiyo, kama ilivyoandaliwa na Sekretariati kuu ya Sinodi.
Askofu Mkuu Nikola Eterovic, Katibu Mkuu wa Sinodi, ametaja idadi ya wajumbe katika sinodi hiyo kwamba, Mababa wa Sinodi ni 262, waliotoka bara zote tano za dunia( Afrika 50, Amerika 63, Asia 39, Ulaya 103 na saba kutoka Oceania). Pia kuna wawakilishi 13 kutoka Makanisa ya Mashariki na wajumbe 114 kutoka Mabaraza ya Maaskofu na Shirikisho linalounganisha wakuu wa Mashirika Katoliki, na wageni waalikwa kutoka makanisa na jumuiya zinazo shirikiana kwa ukaribu na Kanisa Katoliki katika mada hii ya Uijilishaji duniani. Pia kuna watalaam 45 na wahariri 49 wake kwa waume watakao kuwepo wakati wa maadhimisho ya Sinodi hii.
Na amerejea maneno ya Yesu" Nendeni basi mkawafanye watu wa mataifa yote kuwa wanafunzi wangu , mkiwabatiza kwa jila la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu . Wafundisheni kushika maagizo yote niliyowapeni . Nami nipo nanyi siku zote , mpaka mwisho wa dahari Mt. 28:19-20, akisema, ni wito unaongoza Sinodi hii ya kawaida ya XIII, katika kutafakari mada ya sinodi: Uinjilishaji mpya kwa ajili ya uenezaji wa Imani ya Kikristo.
Ni kuhusu utangazaji wa habari njema, iliyohubiriwa na mitume na kudhaminishwa na Mama Kanisa, yaani: kumtangaza Kristo aliyekufa kwa ajili ya dhambi za binadamu, kama ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu, kwamba alikufa na kuzikwa, siku ya tatu akafufuka kwa utukufu na kujionyesha kwa Kefa na mitume wake kumi na waili. Injili inayobaki kuwa ileile na haibadilishwi na utendaji wa binadamu wenye kubadilika badilika katika maisha yake ya kidini, kitamaduni na mipangilio yake ya kijamii, katika namna za kuliishi Neno hili la Wokovu linalohitajika kufikishwa kwa kila binadamu.
Na hivyo katika mkutano huu, Mababa wa Sinodi watachambua kwa kina, haja ya kuwa na mbinu mpya za uinjilishaji kwa ajili ya kuifikisha habari hii njema ya wokovu kwa kila binadamu. Na pia Mababa wa Sinodi watafanya takari hizo sambamba na kutangazwa kwa mwaka wa Imani na maadhmisho ya miaka 50 ya Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican na pia miaka 20 ya kuchapishwa kwa Kateksimu Katoliki.
Askofu Mkuu Nikola Eterovic,ameeleza na kuuweka mkutano huu katika neema za Roho Mtakatifu ili kwamba, Mwaka wa Imani uweze kuwa na zawadi nyingi za kiroho kwa Kanisa la Mungu, Mama wa Waamini.
Na ametoa muhtasari wa Mkutano wa Sinodi hii kwamba kazi zake zitafanyika chini ya vipengere vinne :
1. Uwasilishaji wa kazi zilizofanyika kati ya mkutano ya Sinodi ya Kawaida ya XII na Mkutano wa XIII. Sinodi ya kawaida ya XII, ilifanyika Oktoba 5-26 , 2008, juu ya: Neno la Mungu, katika Maisha na Utume wa Kanisa. Mwisho wa Sinodi hiyo, Maaskofu waliunda sekretariat yenye wajumbe 15 kwa ajili ya kutazama kwa makini yaliyojadiliwa katika sinodi hiyo . Kazi hiyo ilifanyika na taarifa yake kutumwa kwa Maaskofu wote hapo tarehe 30 Mei 2009.
2. Kazi zilizofanyika katika maandalizi ya Sinodi ya kawaida ya XIII, ambayo ni matokeo ya mtazamo mpana wa mashauriano katika taratibu za utume wa kanisa duniani na katka kujali kazi za kichungaji za Papa , Askofu wa Roma na Mchungaji mkuu wa Kanisa la Ulimwengu. Maandalizi mwongozo kwa ajili ya Mkutano wa XIII wa Sinodi ya Kawaida, yalianza mara baada ya Papa kutangaza mada ya majadiliano kabla ya kuchapishwa rasmi.
3. Kutazama shughuli zilizofanywa na Sekretarit Kuu, tangu Octoba 2008 hadi leo, mabamo kwa ombi pa Papa , Sekretariat iliandaa Mikutano ya sinodi mbili maalum , kwanza kwa ajili ya Afrika tarehe 4-25 Oktoba 2009 , na pili kwa ajili ya Mashariki ya kati ya tarehe 10-24 Oktoba 2010.
Na mwisho, Mababa wa Sinodi watajadili Yesu Kristo , Muinjilishaji Mkuu wa kwanza , wakilenga Mada ya Sinodi XIII; Uinjilishaji Mpya kwa ajili ya Uenezaji wa Imani ya Kikristu. Kama ilivyokuwa kwa mitume, katika chumba cha juu wakiwa na Mama wa Yesu, mama wa Kanisa na nyota ya Uinjilshaji ,baada ya kushukiwa na Roho Mtakatifu walitawanyika wote kwenda kuitangaza habari njema kwa watu wote.Hilo ndilo lengo la sinodi hii.
Na kazi zake zimedhaminishwa katika usimamizi wa Mtakatifu Yohane wa Avila na Mtakatifu Hildegard wa Bingen , walimu wapya wa Kanisa, ili kazi hii iwmeze kutoa matunda bora ya neno la Yesu Kristu , Mchungaji mwema" tena ninao wanakondoo wengine ambao hawamo zizini humu. inanibidi kuwaleta hao pia, nao wataisikia sauti yangu na kutakuwapo kundi moja na mchungaji mmoja (Yn.10:16).








All the contents on this site are copyrighted ©.