2012-10-01 15:14:40

Kanisa lashambuliwa kwa bomu Nairobi Kenya


Jumapili , mtoto mmoja alifariki na wengine kadhaa kujeruhiwa walipokuwa wamekusanyika kwa ajili ya Ibada na masomo ya Jumapili, katika Kanisa la Mtakatifu Polycarp, katiak barabara ya Chai, eneo la Eastleigh, Nairobi Kenya. Maafa hayo yalisababishwa na watu kadhaa wasiojulikana kutupa bomu katika kanisa la hilo.
Polisi Kenya wakithibitisha tukio hili wanasema, Waliojeruhiwa wengi wao ni watoto waliokuwa wakishiriki katika masomo ya Jumapili , na walikimbiza ktiak hospitali ya Guru Nanak , baadhi walitibiwa na kuruhusiwa kurudi nyumbani na wengine kulazwa kutokana na hali zao kuwa mbaya. Watoto wengine walijeruhiwa kutokana na hali ya kukanyagana baada ya bomu hili kulipuka, majira ya saa nne na nusu za asubuhi siku ya Jumapili. .
Watu watatu mara walitiwa mbaroni wakati wakijaribu kuchukua picha za tukio hili, ambao wameiambaia polisi kwamba ni wafanyakazi wa Televisheni ya Somalia. Hali ya mvutano mkali ulijitokeza katika eneo hilo, baada ya vijana waliokuwa wamekasirishw ana ulipuaji wa bomu hilo, kuanza kuushambulia msikiti wa Alamin ulio karibu na kanisa lililoshambuliwa lakini polisi waliweza kutuliza ghasia hizo na kuwataka watu wabaki tulivu.
Mwezi Julai , watu 14 waliuawa na wengine 66 kujeruhiwa kufuatia mashambulio mawili pacha katika katika mjini Garissa Kenya








All the contents on this site are copyrighted ©.