2012-09-26 16:01:02

Wakristu Nigeria , hawaogopeshwi na mashambulio ya kighaidi Makanisani- asema Mhashamu Askofu Mkuu Ignatius Kaigama.


“Ukweli ni masikitiko makubwa pamoja na kuwa kulikuwepo na ulinzi lakini walipata namna ya kuweza kuwashambulia na kulipua waamin waliokuwa wakisali jumapili iliyopita”, hayo yalisemwa na Askofu Mkuu Ignatius Ayau Kaigama Rais wa Baraza la Maaskofu nchini Nigeria, wakati akizungumza na shirika la habari la Fides, juu ya bomu lilipuliwa jumapili katika kanisa kuu katoliki la Buachi kaskazini mwa Nigeria. Bomu hilo lililipuliwa na mmoja wanaharakati wa kiislamu wasiovumilia wengine , kikundi cha kigaidi cha Boko haram.

Askofu Mkuu Kaigama, ameyaita mashambulio haya kuwa ya kusikitisha maana mtu huwezi kuwa na uhakika wako wapi, na kwa nini wanafanya hivyo, maana wakati wote wanaweza kujitokeza. Alisema hayo akiwa anaelekea kuwaona waamini wake na hakuwa na uhakika kama atarudi nyumbani kwa sababu watu wakatili wa namna hii wanaweza kufanya chochote kibaya lakini hata hivyo alisema kuwa inabidi kuendelea mbele katika maisha yao na shughuli zao za kila siku bila kuogopeshwa na ugaidi huo.

Mashambulizi mengine yalitokea huko katikati ya wiki iliyopita aliyekufa ni kijana na mwanamke mmoja pamoja na huyo mtu aliyelipua hilo bomu kwa makusudi akiwa ameweka bomu ndani ya gari lake lililokuwa limeegeshwa karibu na mlango wa ulinzi nje kidogo ya kanisa kuu.

Kuhusiana na mashambulizi hayo ya kigaidi Askofu Mkuu Kaigama anaeleza kuwa kundi la kiislam la Boko haram, lililoibuka tangu mwaka 2010 limeshaua watu 1,400 katika mashambulizi yaek sehemu mbalimbali, kanisani, ofisi za serikalini na katika majumba ya ulinzi au masoko.









All the contents on this site are copyrighted ©.