2012-09-22 14:07:30

Papa kuwa na ratiba nzito Octoba na Novemba- Vatican


Baba Mtakatifu Bendikto XV1, kwa mwezi Octoba na Novemba, ana ratiba nzito, kama ilivyotajwa na Ofisiya Liturujia za Kipapa. Shughuli zimeongezwa na uwepo wa Mkutano 13 wa Sinodi ya Kawaida ya Maaskofu, kufunguliwa kwa mwaka wa imani, na ibada ya kutaja Watakatifu Wapya.
Mkuu wa liturujia za Kipapa, Mons. Guido Marino, ameeleza wakati akitoa ratiba ya liturujia zitakazoongozwa na Papa katika kipindi cha mwezi Octoba na Novemba 2012, akisema, Ibada za Misa na sala za kuombea sinodi zitakazo tolewa, ni matukio muhimu, ni wakati wa neema na mwanga wa Kanisa.
Papa anaianza ratiba hapo Alhamis 4 Octoba, atakapo tembelea Madhabahu ya Loreto ambako anakwenda kupiga magoti mbele ya Madhabahu ya Mama Bikira Maria kuomba msaada wake kwa ajili ya baraka za mwaka wa Imani.
Tarehe 7, ambayo ni Jumapili ya XXV11,majira ya saa tatu na nuzu za asubuhi ataongoza Ibada Katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro kwa ajili ya kufungua Sinodi ya Kawaida ya Maaskofu ya 13, ambamo pia atawatangaza rasmi kuwa walimu wa Kanisa, Mtakatifu Yohane wa Avilla na Mtaktifu Ildegarda wa Bingen.
Alhamis 11 Octoba, Papa ataongoza Ibada ya Misa katika Uwanja wa Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro majira ya saa nne za asubuhi, kwa nia ya kuufungua mwaka wa imani.
Na tarehe 21 Octoba ambayo ni Jumapili ya XXIX ya mwaka, Papa ataongoza Ibada ya Misa katika uwanja wa Kanisa Kuu la Mtaktifu Petro majira ya saa tatu na nusu , kwa nia ya kuwataja kuwa Watakatifu, Wenye heri wafuatao: - Giacomo Berthieu- Pedro Calungsod,- Giovanni Battista Piamarta,- Maria del Monte Carmelo Sallés y Barangueras,- Marianna Cope.- Caterina Tekakwitha Anna Schäffer.
Tarehe 28 Octoba, ambayo ni Jumapili XXX, Papa ataongoza Ibada ya Misa katika Altare ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro kwa nia ya kufunga Sinodi ya Maaskofu ya 13.
Na tarehe 2 Novemba, Papa atatolea sala zake akiwa katika mapango ya Vatican ambako atawakumbuka Marehemu wote na Mapapa Marehemu .
Jumamosi tarehe 3 Novemba , saa tano na nusu, Papa ataongoza Ibada ya Misa katika Altare ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro kwa nia ya kuwaombea Makardinali, Maaskofu Wakuu na Maaskofu, waliofariki ktika kipindi hiki cha mwaka mmoja.








All the contents on this site are copyrighted ©.