2012-09-19 16:26:28

Kanisa la Mashariki si makumbusho bali ni hai


Uwepo wa Kanisa Mashariki ya kanisa si kama makumbusho ya kihistoria bali ni li hai. Ni maoni ya Muadhama Kardinali Leonardo Sandri, Mkuu wa shirika kwa ajili ya makanisa ya Mashariki ya Kati, aliyoyatoa baada ya kukamilika kwa ziara ya Kitume ya Papa Benedikto XV1, mwishoni mwa wiki 14-16 Septemba 2012.
Kardinali Sandri, akijibu maswali ya wanahabari juu ya ziara hii ya Papa anasema , ilikuwa ni furaha kubwa kwa watu wa Mashariki ya Kati kuwa karibu na Papa katika siku hizo za kihistoria, ziara iliyowawezesha dunia kuipata picha ya kundi dogo la waumini, kuendelea kubaki imara, bila kutishika, ndani ya kundi kubwa la wamini wa imani nyingine.
Kardinali Sandri amekiri kwamba, Kwa hakika Papa Benedikto XV1, ameweza kulionyesha tumaini la Kanisa lisilo dhoofishwa na hali ngumu wala changamoto za kidunia. Na kwamba bado kuna uwezekano wa kuushuhudia kwa pamoja, upendo Kristu na kanisa lake kwa kwa watu wote, na kuendelea kutembea pamoja katika hali hizi ngumu.
Katika siku hizi za ziara ya Papa , Papa amewezesha kuionyesha sura ya Kanisa hai la Wakristu Waotodosi mbele ya kundi kubwa la Waislamu Mashariki ya kati . Kanisa lililo tayari kuushuhudia Upendo wa Mungu, Kanisa linalojishughulisha na majiundo ya maisha yenye ukweli na upendo kwa kila mmoja hasa kwa lika la vijana, kama inavyojionyesha katika uwepo wa shule za Kanisa, ambazo milango yake i wazo kwa wote.
Na akiziungumzia wimbi la Wakristu kuikimbia Mashariki ya kati , Kardinali Sandri , alirejea himizo lililotolewa na Papa , kuona umuhimu wa kuimarisha mshikamano na Wakaristu wote , hasa katika ufanikishaji wa mahitaji msingi katika yote mawili, maisha ya kawaida na maisha ya kiroho kwa watu wa Mashariki , kama hatua ya kupunguza ukali wa mateso na mahangaiko ya kimwili.
Na kwamba, kunahitajika kuwa na majadiliano ya kina juu liturujia, kati ya makanisa Katoliki na makanisa mengine, kwa ajili ya ufanikishaji wa muugano thabiti zaidi kwa wafuasi wa Kristu, bila kuathiri utambulisho wa liturujia kwa kila Kanisa. Na hivyo kuna haja ya Mapatriaki na viongozi wa makanisa mengine kujadili kwa kina suala hili. Kardinali Sandri ameeeleza na kukiri kwamba njia hii ni ndefu, lakini ndiyo mwanzo, akiutaja mkutano utakaofanyika Desemba kwa ajili hiyo.








All the contents on this site are copyrighted ©.