2012-09-16 15:12:28

Papa ahimiza kuujua utambulisho wa Kweli wa Kristu na kutembea nae.


Jumapili hii macho ya Kanisa la Ulimwengu na dunia kwa ujumla yalielekezwa katika uwanja wa Waterfront, Beirut, ambako Baba Mtakatifu Benedikto XV1, aliogoza Ibada ya Misa majira ya asubuhi. Na baada ya Ibada alikabidhi rasmi Waraka wake wa Kitume kama matokeo ya sinodi ya Maaskofu aliyoiitisha maalum Desemba 2010, kwa ajili ya kutazama hali halisi za maisha Kanisa Mashariki ya Kati. Ibada hii ilihudhuriwa na maelfu ya watu na ilifanyika katika hali ya utulivu na amani.
Katika homili yake Papa, ametoa shukurani zake za dhati kwa viongozi wote wa Kanisa na serikalina kwa mkoa wote wa Mashariki ya Kati, kwa ukarimu wote waliomtendea tangu alipowasili katika taifa hili la Lebanon.
Alisema, “Nawasalim Mababa na Maaskofu wa Makanisa ya Mashariki, mikoa ya jirani, na Makardinali na Maaskofu ambao wamekuja kutoka nchi nyingine. Nawasalimu nyote kwa upendo mkubwa, Ndugu wapendwa kutoka Lebanon na kutoka katika mkoa huu mpendwa wa Mashariki ya Kati, kwa ukarimu wenu wa kujiunga na Halifa wa Petro, kumwadhimisha Yesu Kristo, aliyesulubiwa, kufa na kufufuka. Salamu zangu pia za heshima zimfikie Rais wa Jamhuri, kwa mamlaka ya Lebanon, na kwa viongozi na wafuasi wa mila nyingine za kidini ambao waliopendezwa kuwa nasi katika Ibada hii”. ...

Baba Mtakatifu akitafakri masomo ya Jumapili hii, aliyolenga zaidi katika kumtambua Yesu Kristu ni nani, kama ilivyoandikwa katika Injili ya Marko 8:27- 30, ambamo Yesu anauliza utambulisho wake wa kweli , wakati akisafiri na wanafuzi wake. “ Na ninyi je, mwasema mimi ni nani(Mk 08:29”).
Papa alisema, Yesu anaulizwa swali hili muhimu , akijua yatakayo mfika baadaye katika maisha yake. Yeye alikuwa anakwenda Yerusalemu, mahali ambako tukio la wokovu wetu lilitokea."Watu wanasema mimi ni nani?" (Mk 08:27). Wanafunzi wake walitoa majibu tofauti tofauti sana: Yohana Mbatizaji, Eliya, mmoja wa manabii!
Amebainisha kwamba, leo hii kama ilivyokuwa wakati wa Yesu, kuna wengi wanaokutana na Yesu njiani, ambao wanashindwa kumkiri kuwa ndiye Bwana, na kutoa majibu mengine. Papa anasema, pengine hali hii ya kushindwa kutoa jibu sahihi , inaweza kuwa msukumo na msaada katika kutafuta njia ya kweli. Ni muhimu kuitafuta njia ya kutembea pamoja na Yesu na kumjua Yeye ni nani.
Ni wale tu walio tayari kumfuata katika njia yake, kuishi katika ushirika pamoja naye katika jamii ya wanafunzi wake, wanao weza kulitoa jibu sahihi, la kweli, kujua yeye ni nani. Hatimaye, Petro, ambaye alikuwa akikaa pamoja na Yesu kwa muda fulani, anatoa jibu lake: "Wewe ni Kristo" (Mk 08:29).
Papa aliendelea kusema, Ni jibu sahihi, lakini kwa ajili ya kuzuia upotoshwaji wa maana ya Kristu, Masiya aliyetarajiwa, Yesu aliona haja ya kufafanua zaidi , kwamba, Yeye ndiye Kristu Masiya aliye,taarajiwa atakaye subiriwa kwa ajili ya kumkomboa binadamu dhidi ya dhambi na mauti. Yesu aliongeza hili, kwa kuwa, alitambua watu wanaweza kutumia kutoa jibu la haraka haraka , Yeye ni Kristu, lakini katika mitazamo na matumaini ya uongo ya kidunia.
Yesu anatangaza kwa wanafunzi wake kwamba, imempasa kuteseka na kuuawa na kisha atafufuka. Yesu anataka kuwaelewesha vyema utambulisho wake wa kweli. Yeye ni mtumishi ambaye anatii mapenzi ya Baba yake, hata kwa kutoa maisha yake. Hii tayari ilitabiriwa na Nabii Isaya kama ilivyosomwa katika kusoma kwanza. Yesu hivyo, anaonekana kuwa kinyume na matarajio ya wengi. Yeye ni masiya anayekubali mateso na kifo na kufufuka.
Wakati wa mateso yake yalipoanza Petro alishtuka na kutaka kutoa jibu la upanga , lakini Yesu anamkanya naye, anakataa kukubali kuwa Mwalimu wake atateswa na kufa! Yesu anawakanya wanafunzi wake , ili watambue kwamba mtu yeyote ambaye atakuwa mwanafunzi wake lazima kuwa mtumishi, na hata kukubali kuyatolewa maisha kwa ajili ya ufalme wa Mungu.

Kumfuatia Yesu maana yake ni kuchukua msalaba wake na kutembea katika nyayo zake, njiani gumu ambayo inaongozwa si kwa nguvu ya kidunia au utukufu lakini , ni hiari na uchaguzi wa mtu katika kuifuta hata katika hali ngumu za kupoteza maisha .

Pia Papa aliutumia muda huo wa mahubiri, kutoa mwaliko kwa waamini na watu wote , kuzingatia kwamba, Octoba,11 2012, unaanza mwaka wa Imani. Ni wakati wa kutafakari kwa kina , nia za kumkiri Yesu Kristu kuwa ndiye Bwana wa Maisha. Ni mwaka wa kuitafakari njia hii uongofu wa dhati. Ni kuwa na muda wa kuzama katika tafakari za ndani zaidi, juu ya imani, katika matazamio ya kuwa na uzima wa milele na kukua katika uaminifu wa Kristo Yesu na Injili yake.
Baba Mtakatifu alikamilisha homilia yake kwa kutolea sala yake maalum kwa Bwana ili mkoa huu mpendwa wa Mashariki ya Kati uweze kuwa mhudumu wa amani na mapatano kwa watu wote.








All the contents on this site are copyrighted ©.