2012-09-15 10:39:57

Papa awasilisha na kutia sahihi waraka wake wa Kitume kwa ajili ya Mashariki ya Kati


Ijumaa 14 Septemba 2012, Kanisa Mashariki ya Kati, lilishuhudia tukio la Baba Mtakatifu Benedikto XV1, kuwasilisha na kutia sahihi waraka wake wa kitume kwa ajili ya Mashariki ya Kati. Uwasilishaji huo ulifanyika mbele ya viongozi mbalimbali wa Kikanisa, Mapatriaki na Maaskofu, na pia viongozi wa kisiasa akiwepo Rais wa Lebanon, Michel Sleiman, pia Rais wa Bunge la Lebanon , Mheshimiwa Nabihi Berri na Rais wa Baraza la Mawaziri, Wajumbe wa Baraza Maalum la Sinodi ya Maaskofu kwa ajili ya Mashariki ya kati , na wawakilishi kutoka taasisi mbalimbali za kidini, kitamaduni na kijamii .
Katika hotuba yake, Papa amewashukuru wote kwa dhati kwa makaribisho mazuri aliyoyapokea katiak mkutano huu uliofanyika katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Paulo , nakwa pia kwa wajubme wa Baraza Maalum la Sinodi ya Maaskofu kwa ajili ya Mashariki ya kati, na uwepo wa wawakilishi kutoka Kanisa la Kiotodosi , Waislamu na Wadruze na pia kutoka jumuiya za kitamaduni na kijamii. Alisema uwepo wao wote unampa idhini ya kutia sahihi katika waraka huu wenye azimio la Kitume kwa ajili ya Kanisa Mashariki ya Kati, ikishuhudiwa kwamba , waraka huu pamoja na kulengwa katika Kanisa la Ulimwengu, una umuhimu wa kipekee katika Mashariki ya Kati yote.
Baada ya salaam na Shukurani, Papa alionyesha pia kufurahia kwamba tukio hili la kukabidhi waraka huo, linafanyika katika tarehe hii, ambayo kila mwaka Mama Kanisa, huadhimisha siku kuu ya Kutukuka kwa Msalaba Mtakatifu, Siku Kuu iliyoanza Mashariki tangu miaka ya 335, kufuatia heshima kwa Kanisa Kuu la Ufufuko lililojengwa katika kilima cha Golgota na Kaburi la Bwana wetu Yesu Kristu, ujenzi uliofanyika wakati wa Mfalme Constatine Mkuu, Mtakatifu anayeheshimwa sana Mashariki ya kati .
Papa akiwasilisha waraka huu, alihimiza usomwe katika mwanga wa Siku Kuu hii ya kutukuka kwa Msalaba, ulio jitokeza kwa Constatino wa Chi- Rho, uliong’ara katika usiku wa kiza , ukiandamana na maneno, "katika Ishara hii ya Msalaba Utapata Ushindi."
Papa amesema, kuna kiungo kisichoweza kutenganishwa kati ya Msalaba na Ufufuko wa Bwana ambao Wakristu hawawezi kukisahau kamwe. Msalaba Mtukufu ni kiungo kinacho tuunganisha na Mungu. Bila kuwa na kiungo hiki cha Msalaba Mtukufu, inamaanisha mateso na kifo ,vinafanya hatima ya maisha ya mtu, kukosa thamani .
Papa aliasa, hivyo kwa Wakristu, Msalaba Mtukufu, ni alama ya muungano kamilifu na Upendo a Mungu usiokuwa na masharti kwa binadamu. Msalaba Mtukufu ni kitendo cha imani, kinachomweka muumini karibu na Mungu. Kutukuza Msalaba, ni katika kuwa na hamu ya kuishi na kuuonyesha upendo huu kailimifu kwa wote. Ni kitendo cha upendo. Na hivyo kuutukuza Msalaba ni aaniha uwajibika katika utendaji wote wa kila siku, utendaji wa kidugu na umoja wa kikanisa. Ni chimbuko la ushuhuda wa kweli wa Mkristu. Na Ni ujenzi wa matumaini.

Papa aliendelea kuitazama hali halisi ya Kanisa Mashariki ya Kati akieleza jinsi Mababa wa Sinodi walivyoziishi hali hali za Kanisa katika eneo hili la Mashariki ya kati , furaha na mahangaiko yake , hali za wasiwasi na mashaka, woga na tumaini la wafuasi wa Kristu katika mataifa ya Mashariki ya kati. Kwa namna hiyo, Kanisa lilieweza kusikiliza kilio cha hali hizo kutoka nyuso za watu hawa wake kwa waume wanaoishi katika mazingira magumu na hatarishi katika yote, kimwili na hata kihali wanaoishi katika hali ngumu za mivutano yenye nguvu katika woga na ukosefu wa uhakika , kwa wale wanaotamani kumfuata Kristu , mwenye kutoa maana kamili ya uwepo wao duniani, ambao kw amara nyingi huzuiwa kufanya hivyo na binadamu wengine.

Papa alitoa maelezo hayo na kuendelea kuwaangalisha katika nyaraka mbalimbali za mitume za Agano jipya , ambazo zinahimiza watu kumtukuza Yule menye kuwa na funguo zote za maisha , Yesu Kristu, Mwana w Mungu aliyemwilishwa na kukaan a binadamu ili aweze kumkomboa na kumpa uzima wa Milele. Papa amehoji kwa neema hizi kwa vipi binadamu ashindwe kumtukuza na kumshukuru kwa ajili ya juhudi zao za kulijenga Kanisa lake na udugu katika usharika na kwa ajili ya mshikamano wa kibinadamu unaopaswa daima kuonekana, kwa wote wanaoitwa wana wa Mungu?

Papa amesema, katika mwanga wa matumaini, Kanisa Mashariki ya Kati huwezesha kufikiri tena juu ya tumaini la baadaye kwa mtazamo wa macho ya Kristu .
Papa akiugeukia waraka aliouwasilisha alieleza kwamba, Kwa mtazamo wake wa kibilia na kichungaji ni mwaliko wa kuzamisha tafakari za kiroho na kikanisa , katika wito wake kiliturujia na katika mtazamo wake wa kuhuisha upya katekesi na agizo lake katika majadiliano, waraka unaonyesha njia kwa ajili ya kugundua upya jambo msingi katika kuwa wafuasi wa Kristu, hata katika mazingira magumu na wakati mwingie kwenye hali za kuumiza ambazo hutoa kishwawishi cha kutaka kupuuza au kusahau kutukuka kwa Msalaba Mtakatifu. Na ni hapo ambapo waamini wanaitwa kusherehekea ushindi huu wa upendo dhidi ya chuki , msamaha dhidi ya kulipiza visasi , huduma dhdi ya ubinafsi, unyenyekevu dhidi ya majivuno, umoja dhidi ya migawanyiko na utengano.
Katika mwanga wa siku kuu hii ya Kutukuka kwa Msalaba, na Katika mtazamo wa azimo la mwisho la Sinodi ya Maaskofu kwa ajili ya Mashariki ya Kati, Papa amehimza wote kutoogopa , kusimama imara katika ukweli na katika utakatifu wa imani, kwamba hiyo ndiyo Lugha ya Msalaba Mtukufu. Msalaba wenye uwezo wa kubadilisha hali ngumu na mashaka na kuwa upendo na matumaini kwa Mungu na jirani.








All the contents on this site are copyrighted ©.