2012-09-14 16:20:49

Baba Mtakatifu aianza ziara ya kitume ya kimataifa ya 24 Lebanon


Kunako majira ya saa tatu za asubuhi Ijumaa hii, Baba Mtakatifu Benedikto XV1, aliianza ziara yake ya kitume ya kimataifa ya 24 nchini Lebanon, ambako atakuwa hadi Jumapili 16 Septemba 2012. Papa aliwasili katika uwanja wa Rafik Beirut majira ya saa sita na nusu za adhuhuri kwa saa za Lebanon.
Madhumuni ya ziara, ni kama mhujaji wa Kanisa na Mashariki ya kati yote, anayepeka ujumbe wa amani, wakati anapokutana na watu mbalimbali, viongozi wa kijamii, viongozi wa kidini na vijana pia. Pia yuko Lebanon kwa lengo la kuwasilisha na kutia sahihi katika waraka wake wa Kipapa, wenye tamko la mwisho la kitume, anao uutoa kama matunda ya sinodi Maaskofu aliyoiitisha, maalum kwa ajili ya Kanisa Masahriki ya Kanisa, Sinodi ya Desemba 2009. Sinodi hii ilitazama na kutafakari kwa kina hali za maisha ya Wakristu katika mataifa ya Mashariki ya Kati.
Waraka alioutia sahihi na kuuwasilisha hivyo ni majumuisho ya maoni ya sinodi hiyo kwa Kanisa la Mashariki ya Kati , na utatumika kama mwongozo kwa Kanisa la Mashariki. Katika siku hii ya kwanza ya ziara, Papa amekuwa na matukio mawili makubwa katiak ratiba yake , kwanza ni Mapokeziyaliyofanyika katika uwanja wa ndege wa Rafik wa Beirut nyakati za adhuhuri, na jioni majira ya saa kumi na mbili saa za Lebanon alitia sahihi na kuwasilisha waraka huo kwa viongozi wa kanisa Mashariki ya kati. -------








All the contents on this site are copyrighted ©.