2012-09-12 14:04:42

Papa ahimiza Utamadunishaji sahihi wa Imani


Baba Mtakatifu Benedikto XV1, amehiza utamadunishaji sahihi wa Imani, ili Injili iwe sehemu ya utamaduni wa watu mahalia, kuishi upendo wa Kiinjili , upendo kwa jirani. Msisitizo huo aliutoa Ijumaa iliyopita, 7 Septemba2012 , aliwahutubia Maaskofu wapya wapatao mia, waliokusanyika katika ukumbi wa Swiss Hall, uliopo, makazi ya Kipapa huko Castel Gandolfo.
Maaskofu wapya wamekusanyika Roma kwa lengo la kuhudhuria kozi ya majiundo ambayo hutolewa kwa Maaskofu wapya wateule,kama inavyoandaliwa na Shirika la Kipapa kwa ajili ya Uinjilishaji wa Watu.
Papa katika hotuba yake kwa maaskofu wapya, alisifu kukua kwa Kanisa barani Afrika Asia, Amerika n a Oceania , akisema, kushirikishana furaha hai na ubunifu katika imani, hasa unaofanywa na Jumuiya za Vijana Katoliki, ni ishara ya tumaini kwa ajili ya mustakhabli wa Kanisa la Ulimwengu RealAudioMP3








All the contents on this site are copyrighted ©.