2012-09-12 14:04:49

Mlei ashuhudia umuhimu wa Kongamano la Walei linaloendelea Yaounde Cameroon


Kongamano la Kimataifa la Walei Wakatoliki , linalo hudhuriwa na washiriki kutoka toka pande mbalimbali za Afrika, Wakatoliki walei na viongozi wao, Maaskofu na Mapadre na watawa pia , linaendelea huko Yaounde Cameroon, kama ilivyoandaliwa na Baraza la Kipapa kwa ajili ya Walei.
Padre Moses Hamugole, Mkuu wa Idhaa ya Kiingereza na Kiswahili Radio Vatican, akishiriki katika kongamano hili, alipata nafasi ya kumhoji Queen Said, Mlei toka Tanzania na Mwana jumuiya ya Mtakatifu Egidio, na anatumegea hisia zake kwamba: RealAudioMP3
Kongamano hili la siku tano , 4-9 Septemba 2012, lilifunguliwa Jumanne kwa Ibada ya Misa, mjini Yaounde Cameroon , na linaongozwa na Mada ” Mashahidi wa Yesu Kristu Afrika leo hii. Ninyi ni Chumvi ya Dunia na Mwanga wa Ulimwengu, lengo lake ni kushirikishana uzoefu wa maisha leo hii katika kuieneja Injili ya Upendo wa Kristu kwa watu wote.
Mkutano pamoja na kushirikishana uzoefuwa maisha na maoni yanatazamishwa zaidi katika waraka wa dhamana kwa Afrika, uliotiwa sahihi na Papa Benedikto XV1 na kuukabidhi kwa Kanisa barani Afrika, kama mwongozo wa kutembea pamoja kiliturujia na kichungaji katika neema za hija ya kanisa barani Afrika. Papa anasema, huu ni wito kwa kila muumini mbatizwa kuwa chumvi ya dunia na mwanga wa ulimwengu. .
Papa amelitaja kongamano hili Walei linaloendelea Cameroon kuwa na umuhimu wake katika kupata mang’amuzi ya uvuvio wa Roho Mtakatifu kwa Mababa wa Sinodi ya Pili ya Maaskofu, iliyoandaliwa Maalum kwa Kanisa la Afrika , Sinodi iliyofanyika Octoba 2009 hapa Roma.
Kwa ajili hiyo, Papa ameonyesha furaha yake, kwa uwepo wa Kongamano hilo la Walei ambamo Walei wanaitwa kwa namna ya pekee kulitumika Kanisa Shamba la Bwana, katika nyakati zetu. Kama pia alivyoeleza Papa Yohane Paulo 11, katika waraka wake wa Kanisa barani Afrika, alioutoa kama matokeo ya sinodi ya kwanza ya Maaskofu iliyoandaliwa maalum kwa Kanisa barani Afrika, Octoba 1994. .
Papa Benedikto XV1, kwa mara ingine amerudia tena kulitaja bara la Afrika kuwa ni Bara la Tumaini, licha ya changamoto zinazo likabili.








All the contents on this site are copyrighted ©.