2009-06-10 09:00:13

Bajeti ya Uganda kuwa ya kiasi: vipaumbele: miundombinu na nishati


Waziri wa fedha wa Uganda Sydda Bbumba amesema, Serikali ya Uganda katika bajeti yake kwa mwaka 2009/2010 inatarajia kuwekeza zaidi kwenye miundo mbinu na nishati, kukiwa na ongezeko kidogo sana la bajeti.

Uganda kwa miaka mingi imekuwa ikiongoza kwa sekta ya utalii na uzalishaji wa Kahawa, lakini kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita huduma na uzalishaji viwanadani umeendelea kuongezeka, lakini sekta ya kilimo ambayo inatoa fursa ya ajira kwa asilimia sabini ya wananchi wa Uganda imedumaa, hasa baada ya wawekezaji kutoka nchi za nje kugundua uwepo wa nishati ya mafuta nchini Uganda, katika mipaka yake na Jamhuri ya Kidemokrasia ya watu wa Congo.

Serikali ya Uganda inatarajiwa kutumia kiasi cha shilingi Trillioni sita nukta mbili saba, sawa na Dolla za Kimarekani Billioni mbili nukta tisa nne. Ufinyu wa bajeti hii unatokana pia na mtikisiko wa uchumi kimataifa pamoja na hali ngumu ya kiuchumi inayozikabilia nchi nyingi wahisani.

Wachunguzi wa mambo ya kiuchumi wanasema, Serikali ya Uganda inapaswa kudhibiti mfumuko wa bei ya bidhaa na huduma. Kilimo kinatarajiwa pia kupewa msukumo wa pekee katika bajeti ya Uganda inayotangazwa siku ya alhamisi tarehe 11 Juni, 2009.







All the contents on this site are copyrighted ©.